Historia ya Uibadhiya

Uislamu ulipokelewa kwa amani nchini Omani, bila kushurutishwa wakati Mtume alipoishi. Mnamo mwaka wa 629 AD Mtume Mohammed alituma barua kwa wafalme wawili wa Omani Abd na Jaifar, wana wa Julanda, walioishi Sohar, akiwasihi wawe wafuasi wake. Walibadilishana wajumbe ili kujielemisha na kufikira juu ya jambo hili, na Abd na Jaifar wakakubali kusilimu kwa hiari yao.

Wafalme wawili wa Omani waliunganisha makabila ya kiarabu na mamlaka ya kisiasa yalibaki katika mikono ya utawala wa ukoo wa Al Julanda, mpaka Omani ilipounganishwa na Basra na Khalifa wa tatu Uthman bin Affan. Ilikuwa ni wajibu wa makhalifa – kwanza Abu Bakr, halafu Umar bin Al Khattab – kuteuwa wajumbe wa Waislamu.

Mapambano makali kati ya Khalifa Ali na Muawiyah, yalizusha farakano iliyokuza falsafa ya Suni na Shia ambazo ni tofauti. Abd bin Al Julanda aliamua kwamba Omani haitafuata falsafa za makundi haya mawili, awali alijaribu sana kuiweka Omani huru kwa utawala wa Umayya. Hatimaye utawala wa ukoo wa kinasaba wa Al Julanda ulilazimishwa kuhamia Afrika, kwani mashambulio ya kijeshi yaliyofanyika, ilikuwa kuwashurutisha wajiuzulu.

Matokeo ni kwamba mahali muhimu pa upinzani wa kisiasa palianzishwa Omani, ili kuupinga utawala mabavu wa Umayya, na kwa muda fulani upinzani huu ulibadilika kuwa filosofia ya Ibadhi.